The House of Favourite Newspapers

Ratiba Ligi Kuu Bara leo

0

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeweka wazi kuwa tayari imekamilisha uandaaji wa ratiba ya michezo ya Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2021/22 na inatarajiwa kutoka wiki hii.

 

Pazia la Ligi Kuu Bara linatarajiwa kufunguliwa rasmi Septemba 25, mwaka huu kwa mchezo wa Ngao ya Jamii utakaozikutanisha timu za Simba na Yanga, mchezo huo utachezwa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

 

Pamoja na maandalizi mengine, TPLB juzi Jumamosi waliandaa semina maalum kwa Wanahabari iliyolenga kuboresha uwasilishaji wa taarifa kwa jamii, semina ambayo ilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

 

Akizungumza na Championi Jumatatu, Ofisa Mtendaji Mkuu wa bodi ya Ligi, Almasi Kasongo alisema: “Tunashukuru Mungu kwa kumaliza vyema msimu uliopita wa 2020/21, tena kwa mafanikio makubwa licha ya kwamba kulikuwa na malalamiko katika baadhi ya maeneo, ambayo tumeyafanyia kazi kuelekea msimu ujao wa 2021/22.

 

“Matarajio yetu msimu ujao tutakuwa na uendeshaji bora zaidi, mpaka sasa tayari ratiba ya michezo yote ya ligi imeshakamilika na tunatarajia siku yoyote kuanzia Jumatatu (leo), tutaitangaza rasmi kwa umma wa wanamichezo hapa nchini.”

JOEL THOMAS, Dar es Salaam

Leave A Reply