The House of Favourite Newspapers

Ratiba Kupokea Mwili wa Mkapa Yabadilika

0

MWILI wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, utawasili moja kwa moja kijijini Lupaso, mkoani Mtwara kesho jioni kutoka jijini Dar es Salaam tayari kwa maziko yatakayofanyika Julai 29.

 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa, wakati akieleza kuhusu maandalizi ya maziko ambayo amesema hadi sasa yamefikia asilimia 80.

 

Byakanwa amesema kuwa ratiba imebadilika ambapo awali mwili ulikuwa ushushwe Uwanja wa Ndege wa Nachingwea mkoani Lindi na kisha upelekwa kijijini kwao, lakini sasa utatolewa Dar es Salaam hadi Lupaso.

 

Amesema taratibu za kuhakikisha kunapatikana malazi na usafiri kwa wageni wote watakaofika bado zinaendelea.

 

Leave A Reply