Ray, JB kupima uzito kesho kabla ya kupasuana
WAKALI wa filamu nchini, Vicent Kigosi ‘Ray’ na Jacob Stephen ‘JB’ wanatarajia kupima uzito kesho Jumamosi tayari kwa pambano lao la kukata na shoka linalotarajia kufanyika Aprili Mosi, mwaka huu (Sikukuu ya Pasaka) kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Ray na JB watapanda ulingoni katika pambano hilo la raundi nane ambalo ni la kumaliza ubishi kabla ya bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Twaha Hassan ‘Kiduku’ kupanda ulingoni kuzichapa na bondia kutoka Malawi, Chimwemwe Tchiota.
Akizungumza mtandao huu, Promota wa pambano hilo, Siraji Kaike alisema kuwa maandalizi ya pambano hilo tayari yameshakamilika na kinachosubiriwa kwa sasa zoezi la kupima uzito litakalofanyika kesho Jumamosi kabla ndonga zenyewe.
“Kila kitu kimeshakamilika kwa upande wa maandalizi, bondia kutoka Malawi ameingia nchini juzi Jumatano tayari kwa pambano ambalo linasubiriwa na wadau wengi kutokana na kuwepo mahasimu wa simba na Yanga ambao ni Ray na JB wakionyesha ubebe ndani ya ulingo.
“Hakuna asiyejua kama Ray ni shabiki wa Yanga na JB ni shabiki wa Simba hivyo mashabiki wa Simba na Yanvga watakuwa na kazi moja ya kuwasapoti watu katika pambano hilo kwa kujitokeza kwa wingi pale kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro,” alisema Kaike.
Nje ya mapambano hayo kutakuwa na mapamabano ya utangulizi ambapo bondia Francis Miyeyusho Chichi Mawe atacheza Baina Mazora , Charles Mashali akitarajia kuzichapa na Man Chuga wakati Epson John ataonyesha umwamba na Deo Njiku huku Seba Temba akitatarajia kumalizana na Msafiri Msafiri.
Stori : Ibrahimu Mussa
Comments are closed.