The House of Favourite Newspapers

Rihanna Arudi Kwenye Gemu Kwa Kishindo

BAADA kukaa kimya kwenye muziki kwa miaka mitatu bila kuachia ngoma yoyote, mwanamuziki wa miondoko ya pop nchini Marekani mwanadada Rihana, amewafurahisha mashabiki zake kwa kuachia wimbo wake mpya ujulikanao kama Private Loving.

Rihanna amekuwa akipata  ujumbe mwingi kutoka kwa mashabiki zake kumtaka msanii huyo aachie wimbo mpya kwa kuwa ni muda mrefu tangia mara ya mwisho alipoachia album yake ya Anti mwaka 2016 ambayo ilikuwa na jumla ya nyimbo 16 lakini bado alikuwa kwenye chati za muziki kutokana na kushirikishwa kwenye nyimbo mbalimbali.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, mwanamuziki Rihanna aliwaambia mashabiki zake wakae mkao wa kula kwani wimbo huo upo tayari, kazi ni kwao wafurahie muziki mzuri.

Image result for rihanna Private Loving. twitter

 

 

 

Comments are closed.