Ronaldo de Lima Anawaza Kumsajili Lionel Messi, CR7
STAA wa zamani wa Brazil, Ronaldo de Lima amefunguka kuwa kama angekuwa na fedha angewasajili Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.
Ronaldo aliwahi kutesa na klabu tofauti kama Inter Milan, Real Madrid, Barcelona, PSV,AC Milan, Corinthians na
timu ya Taifa ya Brazil.
Cristiano kwa sasa ana miaka 36 na anakipiga ndani ya Manchester United, huku Messi akiwa
na miaka 34 akicheza Paris Saint-Germain.
Mkongwe huyo anamiliki timu ambayo ilikuwa inashiriki La Liga msimu uliopita na sasa imeshuka daraja ambayo
ni Real Valladolid.
Pia ana timu nyingine kwao Brazil inafahamika kama Campeonato Brasileiro inayoshiriki Serie B na Cruzeiro.
Ronaldo anasema:“Natamani kuona siku moja kama ningekuwa na fedha ningeweza kuwasajili wote wawili. Lakini nafikiri nitamsajili Messi.”
STORI: SÃO PAULO, Brazil