The House of Favourite Newspapers

Saidi Ntibazonkiza Aliyeifunga Stars Atua Yanga

0

Klabu ya Yanga imemsajili Saidi Ntibazonkiza (33) kutoka nchini Burundi. Nyota huyo amesajiliwa na Yanga Oktoba 12 akiwa ni mchezaji huru. Ntibazonkiza ndiye aliyeifungia Burundi goli katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Tanzania (0-1) uliochezwa Oktoba 11, 2020 jijini Dar es Salaam.

“Mkataba wake ni wa mwaka mmoja na nusu, na ataanza kuutumikia Novemba 15, 2020,” amesema Hersi Said kuhusu usajili wa Ntibazonkiza.

 

Msimu wa 2019 alipata dili la kujiunga na Vital’O ya Burundi ila hakuweza kucheza. Miongoni mwa timu ambazo amecheza winga huyo ni pamoja na Kaysar Kyzylord alicheza mechi 10 na kufunga mabao mawili.

Safari ya winga mpya wa Yanga SC Saidi Ntibazonkiza

2003-05 – Vital’O
2005-10 – NEC
2010-14 – Cracovia
2014-15 – Akhisar Belediyes
2015-16 – Caen
2015-16 – Caen B
2017-17 – Kaysar Kyzylorda
2019-20 – Vital’O
2020 Yanga Sc.

Leave A Reply