Sanch: Mwanaume Rijali Anayemtaka Kimapenzi Awe Tayari Kufanya Hivi – Video
MWANAMITINDO maarufu anayetikisa Bongo kwa sasa kutokana na picha zake za utupu, Jane Rimoy ‘Sanch’, amefungukia bila chenga akitaja vigezo vya mwanaume ambaye anahitaji kuwa naye kimapenzi. vifuatavyo.
Akipiga stori na Global TV Online, Sanch alisema;
“Kwanza napenda mwanaume anayejishughulisha, anayejituma, siyo lazima awe na kipato kikubwa sana, lakini awe anajitahidi awe na malengo ya kufika mbali zaidi. Cha pili anikubali nilivyo na anisapoti” alisema Sanch.
Aidha aliongeza kuwa tangu azaliwe hajawahi kumtongoza mwanaume huku akidai kuwa hajawahi kuvutiwa kimapenzi na mastaa wa Bongo, lakini anavutiwa zaidi na msaniii maarufu wa Marekani, Drake.
Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers
Android ===>Google Play
iOS ===>Apple Store
==