The House of Favourite Newspapers

SANCHI AFUNGUKIA KUKODI NDEGE

Jane Rimoy ‘Sanchi’

BAADA ya kusemekana kukodi ndege binafsi akitokea Dar kuelekea mkoani Iringa, mwanamitindo maarufu Bongo, Jane Rimoy ‘Sanchi’ amefunguka kuwa hajawahi kukodi ndege zaidi ya kupanda kama abiria wengine. 

 

 Akizungumza na Za Motomoto, Sanchi alisema kuwa, alipiga picha tu kama wanavyopiga watu wengine wakishuka kwenye ndege, lakini siyo kwamba alikodi na pia bado hajafikia hiyo hadhi ya kukodi.

 

“Siwezi kukodi ndege bana, hiyo ilikuwa na abiria wengi tu na mimi nilikuwa ni mmoja wa abiria ila nilipiga picha wakati watu wameshuka ikaonekana nipo peke yangu,” alisema Sanchi.

Stori: Imelda Mtema

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO


Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.