The House of Favourite Newspapers

SANCHI: SIHITAJI MWANAUME WA KUNIOA

MWANA-MITINDO maarufu Bongo, Jane Ramoy ‘Sanchi’ ametoa la moyoni kuwa hahitaji mwanaume wa kumuoa kwa hivi sasa na kama angetaka, wapo wengi wamepanga msururu.

 

Mrembo huyo amefunguka hayo baada ya mitandao ya kijamii hivi karibuni kumuandama kuwa, iweje yeye ana ‘mzigo wa haja’ haolewi wengine ambao hawana hata shepu wanaolewa kila kukicha.

 

Kufuatia maneno hayo mtandaoni huku wengine wakipingana nayo kwa kusema siyo kila mwenye shepu ana haki ya kuolewa, Sanchi alisema:

 

“Jamani naomba watu wajue kabisa mimi sihitaji kuolewa kwa sasa, ningekuwa nataka kuolewa ingekuwa zamani, wapo wanaume wengi wanataka kuleta posa kwetu lakini sasa hivi nimesema hapana kwanza.”

IMELDA MTEMA 

Comments are closed.