The House of Favourite Newspapers

Shabiki wa Rooney Akutana na Championi

0
Shabiki Hassan Omary, akiingia katika Uwanja wa Taifa.

UNAMKUMBUKA yule shabiki ambaye Alhamisi iliyopita aliingia uwanjani na kumkumbatia straika wa Everton, Wayne Rooney? Basi amekutana na Championi na kufunguka mambo kadhaa kwa ufupi.

Shabiki huyo anayefahamika kwa jina la Hassan Omary, aliingia katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati Everton ilipokuwa ikipambana na Gor Mahia ya Kenya ukiwa ni mchezo maalum wa kirafiki ulioandaliwa na Kampuni ya Michezo ya Kubashiri ya SportPesa ambapo Everton iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Akiwa kamkumbatia Rooney.

Jana Jumapili, shabiki huyo alikutana na Championi maeneo ya Kibaha Picha ya Ndege ambapo ndipo anapoishi huku akisema alipanga kufanya tukio lile kutokana na mapenzi yake kwa straika huyo wa zamani wa Manchester United.

“Kwa kweli nilipanga kufanya tukio lile, ila kwa sasa siwezi kuzungumza zaidi, kesho (leo Jumatatu) nitakuja ofisini kwenu na nitazungumza yote kupitia runinga yenu ya Global TV Online ili watu wengi waweze kuniona na kunisikia,” alisema shabiki huyo. Subscribe Hapa www.youtube.com/user/uwazi1

Stori: Ibrahim Mussa na Abdallah Zalala | Championi

Leave A Reply