The House of Favourite Newspapers

Sheria Ngowi Aiomba Serikali Ipunguze Uingizwaji wa Mavazi ya Nje

0
 Sheria Ngowi akifanyiwa mahojiano na +255 Global Radio.

MBUNIFU maarufu wa mavazi na mitindo wa kitaifa na kimataifa, Sheria Ngowi, ameiomba serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Habari, Sanaa na Michezo kupunguza uingizwaji wa mavazi ya nje.

Sheria Ngowi akizungumza na Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho (kushoto), katikati ni Meneja wa Vipindi wa +255 Global Radio.

Sheria amesema jambo hilo litasaidia kuinua soko la  wabunifu wa mavazi wa ndani ya nchi ili kukuza kipato na pato la taifa kwa ujumla.

Mhariri Kiongozi wa Global Publishers, Richard Manyota akimwelekeza jambo Ngowi.

 

Sheria amesema jambo hilo litasaidia kuinua soko la  wabunifu wa mavazi wa ndani ya nchi ili kukuza kipato na pato la taifa kwa ujumla.

Ngowi akisalimiana na Mhariri Mtendaji wa Global, Saleh Ally ‘Jembe’.

Mkali huyo wa mavazi amesema kuwa bila serikali kuweka mkono wake katika masuala ya sanaa, wasanii hawatafikia malengo kutokana na masoko yao kuyumba.

Ndani ya studio za  Global Radio.

 

Aidha, amesema ni vizuri likawepo Vazi Rasmi  la Taifa ili kuweza kuwatambulisha Watanzania pale linapokuja suala la ubunifu kwani kila kabila hapa nchini lina vazi lake rasmi la asili, hivyo ingependeza kuwepo na vazi la taifa litakalowakilisha mavazi ya makabila yote.

Mkuu wa Global TV, Kelvin Nyorobi akimfafanulia jambo Ngowi.

 

Pia, mbunifu huyo amewashauri vijana kuendelea kujituma katika kutimiza ndoto zao na kutoogopa changamoto ambazo wanakutana nazo katika kutimiza ndoto zao.

 

Amesema yeye binafsi ni mmoja kati ya watu ambao kwa miaka saba ameweza kufanya kazi za ubunifu na ameshikilia nafasi ya kwanza Barani Afrika na kuchukua tuzo za ubunifu wa mavazi duniani mara 44.

Mkuu wa Idara ya IT, Edwin Lindege akisalimiana na Ngowi.
Wasanifu Kurasa, Bahati Haule (kulia) na Huruma Bujiku wakimwelekeza jambo Ngowi.

 

Msanifu na Mhariri Video wa Global TV, Robert Azgard akimwelekeza jambo Ngowi.

 

Ngowi nje ya Studio za Global Radio.

 

Ngowi akiwa na watangazaji wa kipindi cha Mid Morning Fresh ya Global Radio.

 

PICHA NA HUSSEIN MANANE | +255 GLOBAL RADIO

Leave A Reply