The House of Favourite Newspapers

Shikalo, Sheva Waipa KMC Jeuri ya Ubingwa

0

 

BAADA ya kukamilisha usajili na kuwatangaza nyota Miraji Athumani ‘Sheva’ na Faroukh Shikalo, Uongozi wa KMC umeweka wazi kuwa malengo yao msimu ujao ni kutwa ubingwa na siyo tu kushiriki.

 

Miraji amejiunga na KMC kwa mkataba wa mkopo wa msimu mzima akitokea Simba, huku Shikalo yeye akijiunga nao kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake ndani ya klabu ya Yanga.

 

KMC msimu uliopita walimaliza katika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara, baada ya kukusanya pointi 48 katika michezo 34, waliyocheza.

 

Akizungumza na Championi Jumatatu, Ofisa Habari wa KMC Christina Mwagala alisema: “Tulikuwa tukiwaambia watu kuwa msimu huu tumefanya usajili wenye hadhi ya Petroli katika kuhakikisha tunashusha nyota wenye uwezo mkubwa na vijana.

 

“Tulianza kwa kumtangaza Faroukh Shikalo ambaye alicheza Yanga msimu uliopita na leo (jana), tumemtangaza Miraji Athumani.

 

“Jambo la muhimu kwa mashabiki wa KMC ni kuwa hatujamaliza bado kuna majembe mapya matano ambayo tunakwenda kuyatangaza.

 

“Tuna imani kubwa kwa msimu ujao nasi tutakuwa miongoni mwa timu zitakazopambania kutwaa kombe la Ligi Kuu Bara.

 

JOEL THOMAS, Dar es Salaam

 

Leave A Reply