The House of Favourite Newspapers

Shilole: Amtesa Nuh kwa tatuu

0

085A4302
Nuh Mziwanda.

Hamida hassan

Kama huna taarifa basi kaa ukijua kuwa, lile penzi lililokuwa na sarakasi nyingi, mara wafumaniane, mara wapigane, mara waachane sasa limefikia mwisho kama siyo kikomo. Nawazungumzia mastaa wawili, Nuh Mziwanda na Shilole ambao wametangaza rasmi kwamba kila mmoja kuwa na hamsini zake.

Shilole amesema kuwa, haoni sababu ya kuendelea na Nuh kwa kuwa anahisi anambana tu na wala haoni faida kubwa ya kuwa naye.

d290401e3271502b498a8052d9897e0fNuh Mziwanda akiwa na aliyekuwa mpenzi wake Shilole.

Kufuatia maneno hayo, Nuh ameona isiwe kesi, amekubali yaishe lakini taarifa iliyotua kwenye ukurasa huu ni kwamba, jamaa anahaha kufuta tatuu aliyojichora mwilini mwake yenye jina la Shilole.

“Kimsingi ile tatuu ya Shilole inamtesa sana Nuh,” alisema rafiki wa msanii huyo.
Nuh anasemaje? Msikie: “Ni kweli ila hii tatuu nitaifuta nitakapompata wa kuziba pengo la Shilole.”

Leave A Reply