The House of Favourite Newspapers

Siku za Msomaji wa Championi Kuibuka na Ndinga sasa Zinahesabika

0
Baadhi ya wasomaji wa magazeti ya Championi na Spoti Xtra wakishiriki kujaza kuponi kwa ajili ya bahati nasibu ya shinda gari.
Msomaji wa magazeti ya Championi na Spoti Xtra akishiriki kujaza kuponi kwa ajili ya bahati nasibu ya shinda gari.
Mkuu wa kitengo cha masoko Globl Publishers, Anthon Adam akiwaelekeza Baadhi ya wasomaji wa magazeti ya Championi na Spoti Xtra namna ya kushiriki kujaza kuponi kwa ajili ya bahati nasibu ya shinda gari.
Mmoja wa wasomaji akimwelekeza mwenzake sehemu inayopatikana kuponi .

Ofisa Masoko wa Global, Songolo Bilal (katikati) akiwaelekeza namna ya kujaza kuponi za kushiriki bahati nasibu ya shinda gari.

Mwanadada akilisoma gazeti la Spoti Xtra.
Wasomaji wakiendelea kuelekezwa na Bilal namna ya kushiriki bahati nasibu hiyo.

Zikiwa zimesalia dakika za lala salama kwa msomaji wa magazeti ya bora ya michezo yanayoongoza kwa habari za uhakika zilizofanyiwa uchunguzi wa kina ,Championi na Spoti Xtra, kujinyakulia gari aina ya Toyota Fun Cargo jana Alhamisi maofisa wa idara ya Masoko na Usambazaji waliendelea kuwasisitiza wasomaji hao kushiriki bahati nasibu hiyo.

 

Kitengo cha Masoko na Usambazaji cha magazeti hayo, jana kiliingia mitaani maeneo mbalimbali ya jiji la Dar ikiwemo Manzese, Magomeni na Mwananyamala na kuzidi kuwahamasisha wasomaji hao kuendelea kushiriki Bahati Nasibu hiyo na kuweza kunyakua gari hilo.

 

Wasomaji hao walionekana kuhamasika na kuonekana kuyachangamkia magazeti hayo na kujaza kuponi inayoelekeza jinsi ya kushiriki shindano hilo.

 

Akizungumza na wasomaji hao, Mkuu wa Idara ya Masoko na Usambazaji, Anthony Adam aliwaambia wasomaji hao kuwa mshindi huyo anatarajiwa kupatikana mapema wiki ijayo.

 

Anthony amesema katika kumsindikiza mshindi wa gari hilo zitachezeshwa droo nyingine ambapo washindi wa zawadi mbalimbali kama vile simu za kisasa za mkononi (smart phone) pesa taslimu na nyinginezo nao watapatikana.

 

Anthony aliwasisitiza wasomaji hao kuchana kuponi iliyopo ukurasa wa pili kwenye magazeti hayo na kumkabidhi muuza magazeti yeyote aliye karibu nao kwa ajili ya kuweza kujishindia gari na zawadi hizo.

 

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL

Leave A Reply