The House of Favourite Newspapers

Simba na Azam Kushiriki Kombe la Muungano baada ya Miaka 20

0

Kwa mara ya kwanza baada ya miaka 20 Kombe la Muungano linarejea tena wakati ambao Taifa linasherehekea maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Taarifa ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) imesema TFF kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) zimetangaza kurejea kwa kombe hilo huku ikibainisha kuwa timu za Simba SC na Azam FC kutoka Tanzania Bara, zitashiriki katika Mashindano hayo ya mwaka huu yenye sura ya Uzinduzi wa Kombe hilo, huku kwa upande wa Visiwani timu shiriki ni mabingwa wa Zanzibar, KMKM pamoja na KVZ FC.

Mechi hizo zitachezwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar kuanzia Aprili 23.

“TFF na ZFF tunawaomba Watanzania wote kushirikiana ili kufanikisha mashindano haya kwa ufanisi na ubora wa hali ya juu.” imesema taarifa hiyo.

Leave A Reply