Simba, Yanga Zapewa Vibonde FA
ROO ya mechi za FA, zimepangwa Jijini Dar es Salaam na kushuhudia timu 64 zikipangwa kwenye makundi mawili ya A na B.
Timu hizo ni za Ligi Kuu,Daraja la Kwanza,Daraja la Pili na washindi wa FA mikoa.
Yanga itakutana na mshindi kati ya Ihefu na Tukuyu Stars zote za Mbeya ambazo zitacheza Jumamosi hii.
Simba watavaana na timu ya Mashujaa FC kutoka Kigoma huku Ruvu Shooting wakimenyana na mshindi kati ya Muccoba FC na Elephant FC kutoka Iringa.
Mechi hizo ambazo zitahusisha vigogo zitapigwa kuanzia Desemba 21 na 24 huku michezo takribani 32 ikifanyika mwezi huu.
Shughuli ya kupanga makundi iliongozwa na viongozi wa TFF jana ambapo Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten alikumbukia walivyowatoa Ihefu kwa penalti msimu uliopita baada ya kwenda nao sare.
Azam FC atacheza na mshindi dhidi ya Madini na Stand Babati.
Comments are closed.