Smirnoff Ice Black Yarudi Sokoni kwa Kishindo
WATUMIAJI wa kinywaji cha Smirnoff Ice Black wana kila sababu ya kufurahi baada ya Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) kukirudisha sokoni kinywaji hicho baada ya kukosekana kwa muda.
Smirnoff Ice Black ni kinywaji kilichochanganywa na kilichopo tayari kwa ajili ya kutumiwa ambacho ni sehemu ya vinywaji vinavyozalishwa na kampuni mama ya SBL, Diageo.
Akiongea wakati wa uzinduzi wa kinywaji hicho jijini Dar es Salaam, meneja uvumbuzi wa SBL Bertha Vedastus alisema kinywaji hicho sasa kitakuwa kinapatikana kila sehemu na kuwataka watumiaji wake kuendelea kukifurahia.
“Baada ya kusubiri kwa muda, sasa tumewaletea tena kinywaji hiki cha kimataifa ili muweze kuendelea kukifurahia, Ni kinywaji chenye ladha nzuri na ya kipekee ambayo unaweza kuifurahia na marafiki,” alisema.
Bertha alisema pamoja na kuwaburudisha watumiaji wake, Smirnoff Ice Black imekuwa ikiunga mkono jitihada za kuendeleza vipaji mbali mbali vya vijana ikiwa ni pamoja na shindano la kusaka vipaji vya Ma-DJ wachanga ambapo tayari limeshafanyika mara tatu kipindi cha Nyuma.
“Kikiwa pia ni kinywaji kinachounga mkono ukuzaji wa vipaji, baada ya kurudi sokoni tutakwenda mbali zaidi kwa kuunga mkono siyo tu kutafuta Ma-DJ bali hata vipaji vingine na kwa hiyo vijana wa Kitanzania waendelee kufuatilia kwa ukaribu ili waweze kusikia na kupata fursa kutoka Smirnoff Ice Black,” alisema.