The House of Favourite Newspapers

Snura: Majanga ilinipa majanga

0

snuramushi

Stori: Gladness Mallya

STAA wa Muziki wa Kizazi Kipya, Snura Mushi ambaye alipata kiki ya aina yake kwa kibao chake cha Majanga, amefunguka kuwa licha ya kupata shoo nyingi kupitia ngoma hiyo, lakini pia alipata majanga kwa kutapeliwa mara kadhaa.

Akipiga stori na Risasi Vibes, Snura alisema promota mmoja alimpeleka kufanya shoo mkoani Kilimanjaro na Mererani Arusha, lakini baada ya kuwa ameshafanya kazi, mtu huyo alimkimbia bila kumpa chake, kiasi kwamba alilazimika kurejea Dar kwa lifti.

“Sitasahau, nilisaidiwa lifti mimi na wacheza shoo wangu kutuleta Dar, lakini baadaye nilikuja kumpata huyo promota, nikamnyang’anya pete ya ndoa na uchumba, ninazo mpaka leo maana hakunilipa,” alisema Snura.

Leave A Reply