Stars Yatakata Benin
TIMU ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars leo Oktoba 10, imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Benin kwenye mchezo wa kufuzu fainal za kombe la dunia 2022, mchezo uliochezwa kwenye dimba la Stade de I’amitie Mathieu Cotonou, Benin.
Goli pekee la Stars limekwamishwa wavuni katika kipindi cha kwanza na Simon Msuva dakika ya 6’ kwa mkwaju mkali uliomshinda mlinda mlango wa Benin.
Kwa matokeo hayo Stars inaongoza kundi J kwa kufikisha alama 7 sawa na Benin wakitofautiana magoli ya kufunga na kufungwa.
Stars imebakiza mechi mbili dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC itakayochezwa Dar, na mechi ya mwisho dhidi ya Madagascar ugenini.