The House of Favourite Newspapers

Tamisemi Yatangaza Nafasi 77 za Ajira kwa Kada za Afya, Maombi kabla ya Julai 22

0

SERIKALI kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR – TAMISEMI) imetangaza tena nafasi za ajira kwa kada za Afya 77 nakuwataka watanzania wenye uwezo na sifa za kujaza nafasi hizo kutuma maombi kabla ya Julai 22, 2023.

Nafasi hizo ni kwa ajili ya Hospitali za Halmashauri, Vituo vya Afya na Zahanati.

Wataalamu wa Kada za Afya wenye sifa wanatakiwa kutuma maombi kwa njia ya mtandao kupitia kiunganishi cha ajira.tamisemi.go.tz. Waombaji ambao waliwahi kutuma maombi yao awali kupitia mfumo huu wanatakiwa kuhuisha (update) taarifa zao na barua za maombi.

Leave A Reply