Na Dustan Shekidele, Morogoro
Dereva wa Kampuni ya Global Publishers, Heladius Banzi amepata pigo baada ya kufiwa na mama yake mzazi, Antonia John aliyefariki ghafla Mei 15, mwaka huu nyumbani kwake, Kigurunyembe, Mzambarauni mjini hapa.
Mama Banzi alifariki ghafla usingizini akiwa na umri wa miaka 89. Marehemu alijaliwa kuwa na watoto 13 ambapo watano kati yao walishatangulia mbele ya haki hivyo ameacha watoto 8, wajukuu 42 na vitukuu.
Mazishi ya mama Banzi yalifanyika jana Jumatano, Mei 17, 2017 katika Makaburi ya Kigurunyembe, jirani na Chuo cha Ualimu cha Kigurunyembe mjini hapa.
PICHA: DUSTAN SHEKIDELE/GPL