The House of Favourite Newspapers

TGNP Yawanoa Kinamama Waliotwaa Udiwani

0
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi (kulia) akifungua warsha hiyo.

MTANDAO wa Jinsia wa TGNP leo Alhamisi umeanza warsha ya kuwanoa kiungozi kinamama kutoka mikoa mbalimbali waliotwaa udiwani na nyadhifa nyinginezo katika uchaguzi mkuu uliopita.

Waheshimiwa Madiwani wakipata somo.

Warsha hiyo iliyofunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi inaendeshwa Makao Makuu ya mtandao huo, Mabibo Jijini Dar, ambapo inatarajiwa kumalizika Jumamosi ijayo.

Mkurugenzi Lilian Liundi akiwahamsisha jambo kwa madiwani hao kinamama ili kufikia usawa wa hamsini hamsini.

Akifungua warsha hiyo Lilian amesema itaendeshwa na walimu wabobezi wa masuala ya uongozi lengo ikiwa ni wanawake nao kufikia usawa wa hamsini kwa hamsini na wanaume katika nafasi za uongozi.

Mheshimiwa Marisea Mamseri Diwani wa Kata ya Rombo mkoani Kilimanjaro akielezea jinsi alivyofanikisha ujenzi wa shule za msingi, sekondari na vyoo vya kutosha na vya kisasa kwenye yake.

Madiwani hao wanatoka katika Halmashauri 24 kutoka mikoa ya Mbeya Mara, Shinyanga, Morogoro, Pwani, Sumbawanga, Kilimanjaro na mingineyo.

Mheshimiwa Rhobi John, Diwani wa Kata ya Kyole mkoani Mara akielezea jinsi alivyokuwa mkeketaji maarufu na kuiasi kazi hiyo ambapo sasa anaongoza mapambano ya kupinga ukatili huo.

Katika warsha hiyo madiwani hao kinamama walijifunza mambo mbalimbali ya kiuongozi na baadhi yao kutoa ushuhuda wa mambo makubwa waliyoyafanya katika maeneo yao.

Mheshimiwa Julitha Maige, Diwani wa Kata ya Kisumwa Rorya mkoani Mara akielezea jinsi alivyoipambania kata yake mpaka kupata vituo vya afya na barabara.

Miongoni mwa madiwani waliotoa ushuhuda wa jinsi walivyopambana kutetea jamii ni Diwani wa Kata ya Mji Mpya iliyopo Manispaa ya Morogoro, Kiwa Rajab ambaye alipambana na kufanikiwa kubadili matumizi ya eneo lililokuwa likitumiwa na wanywaji wa pombe za kienyeji na kujengwa Zahanati inayotoa huduma mbalimbali ikiwemo kliniki ya wamama na watoto.

Waheshimiwa madiwani wakiwa kwenye pozi la ushindi wa hamsini kwa hamsini na Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi mwenye (miwani katikati).

Madiwani hao walitoa shuhuda mbalimbali za mambo makubwa waliyoyafanya ambayo hapo awali madiwani waliopita walishindwa kuthubutu kuyafanya.

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL 

Leave A Reply