THEA, MIKE SANGU MAHABA BADO YAPO
MASTAA wa filamu za Kibongo, Mike Sangu na Salome Urassa ambao walikuwa ni mume na mke kabla ya kutengana kwa muda mrefu, juzikati walionesha kuwa bado wanapendana kwa kuitana majina matamu, kitu ambacho kiliwaacha wengi midomo wazi.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na Ijumaa Wikienda, lilichukua nafasi maeneo ya Yombo Dovya jijini Dar ambapo wasanii hao walikwenda kutoa msaada kwa Hamisi, mtoto anayesumbuliwa na uvimbe.
Ilikuwa hivi; wakiwa eneo hilo mmoja wa wasanii alimtania Thea na kumwambia kuwa, Mike anamuita. Bila kutarajia Thea alimsogelea Mike na kumuuliza kwa sauti iliyotokea puani; ‘Eti kweli unaniita mume wangu?’
Maneno hayo yaliyotoka kwa sauti ya kimahaba yaliwafanya wasanii waliokuwa eneo hilo kuamini kuwa bado wawili hao wanapendana na huenda siku moja wakarudiana kwani waswahili wanasema; penzi la kweli halifi.
STORI: Imelda Mtema, Ijumaa Wikienda
Comments are closed.