Tibu UTI kwa kutumia Baking Soda na siki ya Tufaha
Wiki hii kwenye safu hii nitaongelea jinsi ya kutibu ugonjwa wa UTI unaowasumbua wanawake wengi, wengi wao hawajui tiba asilia ya kumaliza tatizo.
Chukua kijiko kikubwa cha Baking Soda kilichojaa changanya kwenye glasi moja ya maji koroga kisha kunywa asubuhi kabla hujaweka kitu chochote tumboni.
Kunywa mara moja kwa siku, au chukua kijiko kidogo cha chai weka kwenye kinywaji unachokipenda kisha kunywa.
Jinsi ya kutumia siki ya tufaha
Chukua vijiko viwili vya siki ya tufaha changanya kwenye glasi ya maji kunywa kwa siku mara tatu kila muda na glasi yake, kunywa maji hayo dakika 20 kabla ya kula.