Tukio la kigaidi… Mastaa kibao waguswa na mauaji!
Beyonce.
MASTAA wa muziki na wanamitindo nchini Marekani wakiongozwa na Madonna, John Legend, Kim Kardashian, Beyonce na wengineo juzikati walionesha kuguswa na tukio la kigaidi lililotokea nchini humo na kuwaua watu zaidi ya 50 ambapo walitumia mitandao ya kijamii kuombeleza.
Kim Kardashian.
Kupitia kurasa zao za Twitter na Instagram waliomboleza kwa kuandika;
“Sala na rambirambi zote kwa wana Orlando,” aliandika Beyonce Instagram.
John Legend
“Nashindwa kuelezea. Kwa wote walioathirika, nipo nanyi kwa upendo na sala,” aliandika Kim Kardashian Twitter.
Mauaji hayo yalitokea Juni 12, mwaka huu baada ya kijana Omar Mateen (29) kuingia klabu ya usiku ya Pulse jimboni Florida na kufyatua risasi zilizosababisha mauaji ya watu wasiopungua 50 na wengine 100 kutekwa.