Twanga Ilivyozindua Albam ya 14 Kibabe, Mashabiki Full Vibe, Nyomi Kama Lote
Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta International’ usiku wa kuamkia leo imezindua albam yake ya 14 iitwayo Mapenzi Sigala Kali “Inawaka mbele na nyuma” huku nyomi kubwa la mashabiki likihudhuria na full vibe.
Uzinduzi huo umefanyika Ukumbi wa Break Point uliopo Kijiji cha Makumbusho Dar ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo Mh. Pauline Gekul.
Twanga kama ilivyo kawaida yao kuingia na sapraiz waliingia na vazi la kiasili na kusababisha mashabiki watumie muda mwingi kutafakari kuanzia mavazi mpaka shoo yenyewe kisha baadae ndipo wakaanza kubadilisha mavazi tofauti na kuinogesha shoo hiyo.
Uzinduzi huo ulikwenda sambamba na kuwatunukiwa tuzo ya keshima wanamuziki waliotukuka wakiwemo walioaga dunia.
Walioibuka na tuzo hizo ni King Kikii, Hassan Bitchuka, Luiza Mbutu na waliopewa tuzo hizo wakiwa wameaga dunia ni pamoja na Abuu Semhando, Banzastone, Mbaraka Mwishehe, Marijan Rajab, TX Moshi William, Aisha Madinda, Ruge Mutahaba, Mcd Tumba na wengineo.
Shoo hiyo iliacha gumzo huku wengi wakipiga mayowe wakitaka irudiwe “irudiweeeee…” Ndiyo mayowe yaliyosikika.
HABARI/PICHA:RICHARD BUKOS GPL