Msaga Sumu
Stori: Andrew Carlos
WAKALI wa nyimbo za Mduara, Singeli, Mchiriku na Bongo Fleva wanatarajiwa kutikisa leo (Aprili 23), ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar katika bonge la shoo lijulikanalo kama Usiku wa Uswazi.
Mkali wa Bongo Fleva, Juma Nature
Akizungumza na Risasi Jumamosi, mratibu wa shoo hiyo, Ester Kiama aliwataja wakali watakaotikisa leo kuwa ni pamoja na mkongwe wa Bongo Fleva, Juma Nature, mkali wa Mduara, Snura, mkali wa Mchiriku Msaga Sumu pamoja na mkali wa Singeli Man Fongo.
“Tutakuwa pia na Kibao Msambwanda ambapo mashabiki wote watakaofika watashuhudia nyonga zikikatwa laivu. Pia tutakuwa na mastaa kibao kutoka Bongo Muvi wakiongozwa na Gabo Zigamba,” alisema Ester.
Shoo hiyo itakwenda kwa kiingilio cha shilingi 7,000 tu getini.
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz