The House of Favourite Newspapers

Utamu Usioisha Hamu -3

0


Ilipoishia…
Monica alishaingiwa na tamaa, alichokifanya ni kuingia bafuni kuoga. Alimuogesha mwenye jina kwa makini sana, huyu akimwambia “Uwe mwaminifu katika ndoa yako, habari za kudanga sitaki, yule nitamchuna tu pesa zake,” ndivyo alivyojiaminisha na kujihakikishia atakuwa mwaminifu katika ndoa yake.
Sasa endelea na chombezo hili…
Alimpenda sana mumewe ingawa hakuwa na pesa za kumtunza akapendeza vizuri, ndiye aliyempatia mumewe mtaji wa kufungua saluni baada ya kuwaomba wazazi wake fedha za biashara.
Kule bafuni Monica alihakikisha ametakata vema mwilini, alipotoka aliingia chumbani ambapo alijipodoa vizuri akijitazama maungoni. Alivaa gauni fupi lililoacha paja zake nono nje. Kila alipojitazama katika kioo alijikubali, ni kweli aliumbika vizuri, na kama ingekuwa mwanamke mzuri kuchagua aina ya mwanaume tajiri, basi Monica asingeweza kuolewa na mwanaume masikini kama mumewe, tena mwenye saluni ya kunyoa na kusuka nywele. Lakini mapenzi hayachagua masikini au tajiri, hakika tajiri anaweza kuachwa akaolewa na masikini, ama masikini anaweza kuachwa akaolewa na tajiri.
Wakati akimalizia kutinda nyusi zake vema, ghafla simu yake ilianza kuita, alipoitazama juu ya kioo, akashtuka.
“Anataka nini sasa hivi?” Aliwaza Monica, mtu aliyekuwa akimpigia ni mumewe wa ndoa kabisa.
Alisonya baada ya kuona hana ujanja, alipokea.
“Niambie mume wangu, pole na kazi…”

“Ahsante, upo wapi?”

“Nitakuwa wapi tena zaidi ya nyumbani…”
“Unafanya nini?”
“Nimetoka bafuni, sasa navaa…”
“Ahaaa, nimekumisi sana mke wangu, usiku wa leo naomba unipe mahaba matamu, leo naamini nitaenjoy sana…”
“Kabisa mume wangu, mwili wangu mali yako…nitaenda kwa mama mdogo kumsalimia nitawahi kurudi…” Monica alisema na mumewe alimpiga mabusu na kukata simu akimwambia asichelewe. Monica alitulia dakika chache alitafakari.
Mara simu yake ikaanza tena kuita, alipoitazama ilikuwa mwanaume tajiri aliyekutana naye nje ya hoteli. Aliipokea akitabasamu.
“Nimemwagiza dereva wangu anakuja kukuchukua, umesema unaishi wapi?”
“Mwambie aje hadi Ubungo maziwa, hapa njia panda…,” alisema, Monica alipomwelekeza akaelewa na kumpatia dereva namba ya Monica.
“Sawa, bosi nitaenda kumchukua…” Dereva Seki alisema.
Alipoiandika namba ya Monica katika simu yake, akashangaa mbona hizo namba anazo na amezisevu jina la mpenzi wake ambaye ni mke wa mtu. Baada ya kugundua hilo kuwa Monica anayetembea naye kumbe anatembea na bosi wake, aliingiwa na hofu kubwa sana. Alibaki ameduwaa, “Weee unachati, nenda haraka sana…nakuomba uende haraka…,” alisema Bosi Mombasa. Ndipo Seki alipongurumisha gari na kuondoka mwendo wa kasi kuelekea Ubungo, alipafahamu hadi nyumbani anapoishi Monica siku zote aliyekuwa akimpenda kuliko kitu chochote.
Uhusiano wa Seki na Monica ulikuwa wa muda mrefu, tangu wakiwa shuleni na walishindwa kuoana kutokana kila mmoja kutaka kubaki na dini yake. Njia nzima, Seki alijiuliza maswali kibao, inamaana Monica anatembea na mwanaume tajiri kiasi hicho, na walikutana wapi na wameshafanya mapenzi kwa muda gani?
“Hivi nikikutana na Monica tu, atashtuka sana maana namfahamu vizuri, ni demu wangu wa muda wote, najiuliza maswali, walikutana wapi na bosi wangu?” Aliendelea kuwaza mpaka alipofika Ubungo maziwa. Lakini kuna kitu kilimjia akilini mwake, akajikuta akibadilisha uamuzi wa kwenda kumchukua Monica.
Wazo lililomjia kichwani wakati huu ni kumpigia simu rafiki yake wa karibu sana aitwaye Sakala.
“Mambo vipi rafiki yangu…”
“Poa, uko wapi?” Aliuliza Seki.
“Nipo Ubungo stendi…”
“Afadhali, naomba uje mara moja hapa Ubungo maziwa njia panda…kuna kazi nataka nikupe…,” Sakala ni fundi magari, siku hiyo hakuwa na kazi yoyote pale Ubungo stendi anapotengeneza mabasi ya mkoani katika kampuni yao Saibaba, hivyo alichukua bodaboda kama alivyoelekezwa na Seki, akaenda kukutana na rafiki yake, hapakuwa mbali sana.
“Vipi braza…,” ndivyo Sakala alivyosema walipokutana na rafiki yake.
“Safi, najisikia vibaya sana…naomba unisaidie …ukamchukue demu wa bosi wangu ukampeleke hotelini…,” alisema Seki, kwasababu Sakala hakujua uhusiano wa kimapenzi na Monica, kwani walifanya mapenzi ya siri na kukutana lodge na walikubaliana hakuna mtu mwingine kuujua uhusiano huo wa wizi na mke wa mtu.
Seki hakutaka kushuhudia Monica wake akienda kumpa mapenzi bosi wake, aliamini asingeweza na pengine angevunja uhusiano wao wa kimapenzi.
Sakala aliridhia, akapewa na namba za simu za Monica, na kadi ya hoteli ambayo angetakiwa kumpatia Monica aweze kuingia hoteli ya kifahari Sinza.Aliridhia, akaingia ndani ya gari huku akiwa amepatiwa elfu ishirini kama ujira wake.
“Demu mwenyewe mzuri?”
“Sijui, weee nenda kamchukue na usimwambie kama nimekutuma mimi, wee mwambie nimetumwa na bosi, na kamwe usinitaje…”
“Kwa nini? Any way poa…,” Sakala aliondoa gari, Seki alihisi kama vile anaumwa, alimpenda sana Monica kuliko kitu chochote, na alifahamu jinsi msichana huyo anavyojua mahaba awapo kitandani. Aliweza kukumbuka mambo mengi waliyofanya na Monica, akatamani kumpigia simu na kumwambia asimpe mapenzi bosi wake, lakini alihisi huenda angeweza kukosa kazi kwasababu ya kutomleta nyumba ndogo ya bosi panapostahili.
***
Sakala alipofika sehemu husika, aliona msichana mzuri akitembea kimahaba na kusimama nje ya gari, akafungua mlango na mwanamke huyo akaingia. Kitendo tu cha kuingia, ndani ya gari harufu nzuri ya manukato ilitawala, alivuta pumzi ndefu. Gari lilikuwa na vioo vya ‘tinted’ ambavyo sio rahisi mtu aliyepo nje kuona aliyepo ndani.
“Mambo kaka…”
“Safi, weee ndo Monica…”
“Yes…umeagizwa na mzee Mombasa?” Sauti laini kama ute wa yai ilisikika, yaani alikuwa mzuri wa kila kitu, sauti, figa, sura, na rangi.
“Mhhh! Amesema nikupeleke hoteli fulani nzuuuriiiii…,” baada ya kauli hiyo, Monica alimpigia simu mzee Mombasa.
“My dear..ameshanichukua ndo tupo njiani tunakuja…”
“Sawa, karibu sana kipenzi changu, nakupenda sana Monica,” sauti nzito ya upole ilisikika.
“Ahsanteeee, nami nakupenda sana…” Monica alizidi kuongea kimahaba zaidi hali iliyomfanya Sakala kugeuza shingo kumtazama mwanamke huyo.
“Dada una sauti nzuri, na sio sauti tu…wewe ni mwanamke mzuri sana…”
“Ahsante, umejuaje kama mi mzuri…”
“Nimekuona, nina uwezo wa kumfahamu mwanamke mzuri, yaani huna kasoro…”
“Ni kweli, ila usijadili sana…maana mi mali ya bosi wako…”
“Ni kweli lakini unaweza kunichunuku….”
“Mmhh! Hapana, siwezi…natembea na wanaume wenye pesa tu…masikini sitaki…labda siku sijafikishwa naweza kumtafuta uweze kunifikisha kilele cha mlima,” alisema Monica, Sakala akacheka.
“Mapenzi hayachagui masikini wala tajiri, sote ni binadamu…siku ukiwa na shida nami nitafute…”
“Sawa, ikitokea…” alisema Monica. Ni mwanamke mzuri lakini hakuwa akiridhika na mwanaume mmoja, mara nyingi amekuwa akichelewa kumaliza ngwe ya kwanza, na ni wanaume wawili tu waliweza kutii kiu yake, naye si mwingine bali ni Seki na Ozaga.
Walienda moja kwa moja hadi hotelini, Sakala alipiga breki na kufungua milango na Monica kabla ya kushuka, alimsogelea na kumnong’oneza sikioni.
“Unajua mapenzi?” ndio swali alilouliza Sakala.
“Ndiyo, najua sana…”
“Kabla ya kuanza mapenzi na mwanamke, ni kitu gani unapaswa kufanya juu ya mwanamke?”
“Kwanza, kabla ya kuanza mapenzi, lazima nimwandae kisaikolojia, nimbembeleze, nimchekeshe…na tunapoingia kitandani, naanza na mabusu ya midomoni, nikitoka hapo nampapasa kifuani, na huwa napenda nimvue nguo mwenyewe…nikishamaliza hilo, lazima nianze utalii wangu wa kujua wapi anasisimka zaidi ili niweze kumgusa sehemu hizo…”
“Basi, inatosha…unaonekana unajua saa…nitakutafuta…alimpigia tena…”
“Naitwa Saka…” alisema kwa kifupi.
“Sawa Saka, nikutakie bahati njema…” Monica alishuka garini na kutembea kimahada hadi mlangoni kisha akaingia hadi mapokezi, alipoonesha ile kadi alipelekwa hadi chumbani, ambapo sasa alikutana na mzee Mombasa akinywa mvinyo taratibu.
Je, nini kitaendelea? Usikose KESHO. Pia kitabu changu cha MAPENZI ASILIMIA 100% Kimetoka, kinauzwa madukani Kariakoo mtaa wa Muhonda. Kwa tsh 12,000/= tu. Pata nakala yako. 0674894889.

Leave A Reply