The House of Favourite Newspapers

VIDEO: IGP SIRRO ALIZA WATU MSIBANI KWA ASKARI 3 WALIOFIA AJALINI JUZI!

ASKARI watatu waliofariki Mkoa wa Kipolisi Rufiji Julai 25, 2019, katika barabara ya Kilwa wilaya ya Mkuranga baada ya gurudumu la nyuma la gari waliyokuwa wakisafiria kupasuka na kupinduka na kusababisha vifo hivyo, wameagwa leo katika Hospitali ya Polisi Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Waliofariki ni Staff Officer I (ACP) Issah Bukuku, Inspector Esteria wa Ofisi ya RCO Rufiji na G 1132 PC Lameck wa Kikosi cha Kuzuia Fujo (FFU) Rufiji.

Majeruhi ni dereva wa gari hilo, F 7167 PC Ibrahim wa Ofisi ya RCO Rufiji na G7651 PC Mgusi wa Ofisi ya RPC Rufiji.

 

Comments are closed.