Maalim Seif Aapishwa Kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar -Video
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi leo Jumanne Desemba 8, 2020 amemuapishwa mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar.
Hafla hiyo inafanyika mjini Unguja, Zanzibar na kuhudhuriwa pia na viongozi waandamizi wa ACT-Wazalendo akiwamo kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe, katibu mkuu, Ado Shaibu na naibu wake, Nassor Ahmed Mazrui pamoja na makamu mwenyekiti- Zanzibar , Juma Duni Haji.
Maalim Seif anakuwa makamu wa pili wa rais wa Zanzibar kwa mara ya pili, mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2010-2016.
⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx