The House of Favourite Newspapers

Mkataba wa Lwandamina Wamalizika Azam, Apewa Shavu

0

LICHA ya kuwa na matokeo mabaya msimu huu Kocha Mkuu wa Azam FC, George Lwandamina ameongezewa mkataba wa mwaka mmoja wa kuzidi kukinoa kikosi hicho. Lwandamina alijiunga na Azam msimu uliopita baada ya kuondoka kwa aliyekuwa kocha mkuu Mromania, Aristica Cioaba.

 

Mpaka sasa Azam imecheza mechi nne za ligi huku akishinda moja dhidi ya Namungo kwa bao 1-0, wakatoka sare na Coastal Union ya 1-1, wakafugwa mabao 2-1 na Polisi Tanzania na Yanga juzi wakawachapa mabao 2-0.

 

Azam pia imetolewa kwenye Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kufugwa bao 1-0 na Pyramid kwenye mchezo wa marudiano baada ya suluhu Uwanja wa Chamazi.

 

Akizungumza na Global Publishers, Ofisa Habari wa Azam FC, Thabiti Zakaria ‘Zakazakazi’amesema kuwa, pamoja na kocha huyo kumaliza mkataba bado wana mpango naye.

 

“Kiukweli sina taarifa kama kocha anataka kufukuzwa ndiyo maana hizo ni tetesi ila hakuna hata mpango wakuondolewa.

 

“Mkataba wake umeisha leo (jana) na kesho (leo), atasaini mkataba mwingine wa mwaka mmoja wa kuendelea kusalia Azam,” alisema ofisa habari huyo.

CAREEN OSCAR, Dar es Salaam

Leave A Reply