Vodacom Watoa Msaada kwa Waathirika wa Mafuriko ya Rufiji na Kibiti
Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom kupitia Taasisi ya Vodacom Foundation, imetoa msaada wa kibinadamu wenye thamani ya takribani shilingi milioni 250 kwa ajili ya waathirika wa mafuriko katika maeneo ya Rufiji na Kibiti mkoani Pwani.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge ndiye aliyepokea msaada huo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Vyombo vya Habari wa kampuni ya Vodacom, Annette Kanora akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele na kuwashukuru kwa msaada huo huku akiziomba taasisi nyingine kuiga mfano wa Vodacom.