VunaDeile Yashirikiana na Mradi wa BBT Kutoa Hamasa kwa Vijana Kujiajiri Kwenye Kilimo
KAMPUNI ya Three Oceans Ltd inayojishughulisha na uendeshaji wa mchezo wa kubashiri wa VUNADEILE imesema itaendelea kushirikiana na serikali katika kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo wa kujiajiri.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Three Oceans LTD, Naseem Allan wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi mbalimbali kwa washindi wanaopatikana kila siku kwenye droo ikiwemo gari mpya aina ya Toyota IST, pikipiki, tv na simu janja aina ya Samsung na iPhone 15.
Ameeleza kuwa katika kuendesha bahati nasibu hiyo, kampuni hiyo inashirikiana na Mradi wa Kilimo wa Building a Better Tommorow (BBT) ili kuhakikisha wanawawezesha vijana.
BBT ni Taasisi iliyopo chini ya Wizara ya Kilimo yenye lengo kuu la kutoa hamasa kwa vijana kujikita kwenye shughuli za kilimo biashara ili waweze kukuza uchumi wao binafsi na taifa kwa jumla.
Kwa upande wake, Mratibu kutoka BBT, Vumilia Zikankura amebainisha kuwa BBT imekuwa ikiwawezesha
vijana kuingia kwenye sekta ya kilimo biashara kwa kuwawezesha mitaji na masoko huku akiwataka vijana kujitokeza kwenye program ya BBT na VUNADEILE Ili waweze kujishindia zawadi mbalimbali.