The House of Favourite Newspapers

Vodacom Yashinda Tuzo 3 za Huduma Bora Kwa Wateja 2023 Zinazotolewa na CICM

0

Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom, mwishoni mwa wiki imetangazwa kuwa mshindi wa tuzo tatu za huduma bora kwa wateja nchini, zilizoandaliwa na kutolewa na Chartered Institute of Customer Management (CICM) jijini Dar es Salaam.

Kampuni hiyo ilishinda vipengele vya kitengo cha utoaji wa huduma bora kwa wateja (mshindi), mtandao bora wa huduma za mawasiliano na intaneti (mshindi wa pili), na uwajibikaji kwa shughuli za kijamii (mshindi wa pili).

Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Kidigitali wa Vodacom Tanzania, Belinda Wera (kushoto) akiwa na Meneja wa Makusanyo, Charles Daniel wakiwa wameshikilia vyeti walivyokabidhiwa baada ya kushinda tunzo za Annual Tanzania Service Excellence Awards 2024 zilizoandaliwa na Chartered Institute of Customer Management (CICM) mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Biashara ya Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi John Ulanga (Kushoto) akiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhi cheti kwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Kidigitali wa Vodacom Tanzania, Belinda Wera (wa pili kushoto) wakati wa hafla ya utoaji tuzo za Annual Tanzania Service Excellence Awards 2024 zilizofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Biashara ya Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi John Ulanga (Kushoto) akiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhi cheti kwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Kidigitali wa Vodacom Tanzania, Belinda Wera (wa pili kushoto) wakati wa hafla ya utoaji tuzo za Annual Tanzania Service Excellence Awards 2024 zilizofanyika jijini Dar es Salaam.
Wageni mbalimbali wakiwa katika hafla ya utoaji tuzo za Annual Tanzania Service Excellence Awards 2024 zilizoandaliwa na Chartered Institute of Customer Management (CICM) na kufanyika jijini Dar es Salaam.
Wageni mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa hafla ya utoaji tuzo za Annual Tanzania Service Excellence Awards 2024 zilizoandaliwa na Chartered Institute of Customer Management (CICM) na kufanyika jijini Dar es Salaam.
Leave A Reply