The House of Favourite Newspapers

Waasi Wateka Vijana Msumbiji

0
Watu wenye silaha wamewateka nyara zaidi ya vijana 100 kutoka kijiji cha Naulala katika Mkoa wa Niassa kaskazini mwa Msumbiji, Shirika la Habari la Lusa limeripoti.
Niassa inapakana na Cabo Delgado, ambayo imekuwa ikikabiliana na waasi wa jihadi tangu Oktoba 2017.
“Kundi la watu wenye silaha limewateka nyara vijana 100 na kuchoma makazi na vibanda katika kijiji cha Naulala, Mkoa wa Niassa, kaskazini mwa Msumbiji,” Lusa limeripoti, likinukuu vyanzo vya Msumbiji.
Vyombo vya habari vya Msumbiji hapo awali viliripoti msururu wa mashambulizi kwenye mpaka wa Cabo Delgado na Niassa ambapo takriban maafisa watano wa polisi waliuawa.
Leave A Reply