Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wakazi wa Wilaya ya Chato, Mkoani Geita mapema leo mara baada ya kuwasili. Rais Dkt Magufuli anawasili wilayani Chato kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa rais.
Wakazi kutoka vitongoji mbalimbali wilayani Chato mkoani Geita, wakiwa wamekusanyika kwa wingi wakisubiri kumsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ambaye amewasili leo mjini humo alikozaliwa.
Wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi kumpokea mtoto wa nyumbani kwao Chato, Mh Rais Dkt. John Pombe Magufuli viwanja vya Mjini Chato mkoani Geita muda huu.