Warembo Miss Tabata 2016 Watembelea Global, Kukwaana Leo
WAREMBO wanaowania taji la Miss Tabata 2016 jana walitembelea ofisi za Global Publishers wachapishaji wa Magazeti ya Championi, Uwazi, Ijumaa, Amani, Ijumaa Wikienda, Risasi pamoja na tovuti hii kuona uzalishaji wa magazeti hayo na shughuli nyingine zinazoendelea ofisini hapo.
Warembo hao watakwaana leo katika shindano litakayofanyika ndani ya Ukumbi wa Da West Park, Tabata jijini Dar ambapo bendi kongwe ya Muziki wa Dansi, The African Stars ‘Twanga Pepeta’ inatarajia kuangusha bonge la shoo.
Warembo watano watakaoshika nafasi za juu katika shindano hilo watashiriki kwenye shindano la Kanda ya Ilala yaani Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania.
Miss Tabata inadhaminiwa na Kampuni ya Global Publishers, Lete Raha, DataStar College, Global Publishers, CXC Africa, Fredito Entertainment, Saluti5 Kitwe General Traders na Bob Entertainment.