The House of Favourite Newspapers

Washindi Benki ya CBA Promosheni ya Weka Amana Wapatikana

0
WASHINDI wa promosheni
Mkuu kitengo cha Masoko wa CBA benki, Solomon Kawiche( Kushoto) akiwaonyesha namba ya mshindi, Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja wa benki hiyo, Hyasinta Mwimanzi (katikati) na msimamizi wa michezo ya kubahatisha nchini,Abdalaah Mrisho, Wakati wa droo ya pili ya promosheni ya ‘Weka Amana Ushinde’ ambapo mkazi wa Dar es Salaam, Dkt. Julieth Kileo alijishindia kiasi cha Shilingi Milioni moja na  kwa upande wa wateja binafsi na wateja wa makampuni ni, Astoni Charles wa kamapuni ya Express chartering and Shiping alijishindia kiasi cha shilingi Milioni mbili.
WASHINDI wa promosheni
Mkuu kitengo cha Masoko wa benki ya CBA, Solomon Kawiche( Katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) .
WASHINDI wa promosheni
Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja wa benki CBA, Hyasinta Mwimanzi(katikati) akiongea kwa simu na mkazi wa Dar es Ssalaam, Aston Charles ambaye alijishindia kiasi cha shilingi milioni mbili. Kushoto ni Mkuu kitengo cha masoko wa benki hiyo, Solomon Kawiche na msimamizi wa michezo ya kubahatisha nchini, Abdalaah Mrisho.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimshuhudia Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja wa benki CBA, Hyasinta Mwimanzi (watatu kushoto)alipokuwa akiongea na mkazi wa Dar es Salaam, Aston Charles ambaye alijishindia kiasi cha shilingi milioni mbili.

WASHINDI wawili wa promosheni ya ‘Weka Amana Ushinde’ kutoka Benki ya CBA leo wamepatikana na kujishindia fedha ambapo mkazi wa Dar es Salaam, Dkt. Julieth Kileo alijishindia kiasi cha Shilingi Milioni moja na kwa upande wa wateja binafsi na wateja wa makampuni alikuwa Astoni Charles aliyeshinda na kupata Sh. Milioni mbili.

 

Hafla hiyo ya droo ya pili ya promosheni hiyo ilishuhudia kukabidhiwa kwa zawadi hizo kukifanyika jijini Dar es Salaam katika ofisi za benki hiyo.

 

Washindi wa zawadi hizo  walielezea furaha yao kubwa kwa kushinda zawadi  na kwamba wataendelea kushiriki huku wakiahidi kuzitumia fedha za zawadi hizo kwa kujiendeleza kimaisha.

 

NA DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply