The House of Favourite Newspapers

Wasomaji Kisarawe Wachangamkia Droo Ya Pili Shinda Nyumba

0

17.Mkazi wa eneo la Kisalawe Mjini (kulia) akijaza kuponi ili kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba. Mkazi wa Kisalawe Mjini (kulia) akijaza kuponi ili kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba.18.Msomaji wa gazeti la Uwazi (katikati) akisoma gazeti lake baada ya kuvalishwa kofia na Ofisa usambazaji wa Global,Jimy Haroub (kulia) kushoto ni muuzaji wa gazeti.Msomaji wa Gazeti la Uwazi (katikati) akisoma gazeti lake baada ya kuvalishwa kofia na Ofisa Usambazaji wa Global, Jimy Haroub (kulia). Kushoto ni muuzaji wa magazeti.
19. Kuponi zikiwekwa kwenye ndoo maalum eneo la Stendi ya Kisalawe kwa ajili ya kushiriki Bahati nasibu ya Shinda Nyumba.

Kuponi zikiwekwa kwenye ndoo maalum eneo la Stendi ya Kisarawe kwa ajili ya kushiriki Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.
20.Msomaji wa Gazeti la Uwazi (kushoto) akielekezwa namna ya kujaza kuponi ili kushiriki Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba. Katikati ni Mwakilishi wa Wakala wa Magazeti ya Global wa Kisarawe, Bethod Ben.
22.Kuponi zikijazwa Kisalawe. Kuponi zikijazwa Kisarawe.23.Kuponi zikiendelea kuwekwa katika eneo la stendi ya Kisalawe ili kushiriki Bahati Nasibu ya Shinda nyumba.Kuponi zikiendelea kuwekwa kwenye ndoo maalum, eneo la Stendi ya Kisarawe.
24. 25.

1.Ofisa Masoko wa Global Publishers,Yohana Mkanda (kushoto) akimvisha kofia msomaji wa Gazeti la Uwazi eneo la Ukonga Dar baada ya kukata kuponi yake ya kushiriki Bahati Nasibyu ya Shinda Nyumba. Ofisa Masoko wa Global Publishers, Yohana Mkanda (kushoto) akimvisha kofia msomaji wa Gazeti la Uwazi eneo la Ukonga Dar baada ya kukata kuponi yake ya kushiriki Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.2.Kofia zikitolewa kwa wasomaji walionunua gazeti na kukata kuponi ili kushiriki droo ya pili. Kofia zikitolewa kwa wasomaji walionunua gazeti na kukata kuponi ili kushiriki droo ya pili.3.Wakipendeza na kofia za Bahati nasibu ya Shinda Nyumba Wakiwa wamependeza na kofia za Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.4.Wakisoma gazeti la Uwazi lenye kipengere cha kukata kuponi kushiriki Bahati nasibu ya Shinda Nyumba. Wakisoma Gazeti la Uwazi lenye kuponi ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.5.Zoezi la kuweka kuponi kwenye ndoo maalum ya bahati nasibu ya Shinda Nyumba likifanyika kwa wakazi wa eneo la Gongo la Mboto Dar. Zoezi la kuweka kuponi kwenye ndoo maalum ya bahati nasibu likifanyika kwa wakazi wa eneo la Gongo la Mboto Dar.6. 7.Ofisa Masoko wa Global,Yohana Mkanda( mwenye kofia) akiwaelekeza namna ya kujaza kuponi ili kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba baadhi ya wakazi wa eneo la Gongo la Mboto. Ofisa Masoko wa Global,Yohana Mkanda (mwenye kofia) akiwaelekeza namna ya kujaza kuponi ili kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba baadhi ya wakazi wa eneo la Gongo la Mboto.8. 9.Wakimzunguka Ofisa Masoko wa Global,Yohana Mkanda (mwenye fulana nyeupe) kutaka kujaza kuponi ili kuweza kushiriki droo ya pili. Wakimzunguka Ofisa Masoko wa Global, Yohana Mkanda (mwenye fulana nyeupe) kutaka kujaza kuponi ili kuweza kushiriki droo ya pili.10 11. 12.Zoezi la kuwavalisha kofia likiendelea baada ya kujaza kuponi ili kushiriki droo ya pili ya Bahati nasiby ya Shinda Nyumba. Zoezi la kuwavalisha kofia likiendelea baada ya kujaza kuponi ili kushiriki droo ya pili ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.13. 14 15. 16

 

WASOMAJI mbalimbali wa magazeti ya Kampuni ya Global Publishers inayochapisha magazeti ya Uwazi, Amani, Risasi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda na Championi, leo wameonekana kuchangamkia droo ya pili ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba wilayani Kisarawe kwa kujaza kuponi na kushiriki.

Maofisa masoko wa Global, walitembelea maeneo tofauti wilayani humo na kugawa zawadi mbalimbali zilizokuwa baada ya kuwakuta wasomaji wakinunua gazeti la Uwazi linalotoka kila Jumanne.

Kabla ya kuingia Kisarawe, maofisa hao walitoa zawadi za kofia kwa wasomaji wa maeneo ya Ukonga, Gongo la Mboto jijini Dar.

Akizungumza na wakazi wa eneo la Kisarawe Mjini, Ofisa Masoko wa Global Publishers, Yohana Mkanda alisema wasomaji wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kununua magazeti hayo na kukata kuponi ili kujinyakulia zawadi nyingi kwenye droo ya pili ya Shinda Nyumba itakayofanyika mwanzoni mwa Februari, mwaka huu sambamba na kujiongezea nafasi ya kushinda zawadi ya nyumba iliyopo eneo la Salasala jijini Dar katika droo ya mwisho.

“Global tumekwisha toa zawadi mbalimbali kwa wasomaji wetu kama vile, fulana, kofia, simu za kisasa, runinga na ving’amuzi vya TING katika droo yetu ya kwanza.

“Niwasihi watu wazidi kununua magazeti yetu na kujaza kuponi ili waweze kushiriki bahati nasibu yetu. Kitu cha muhimu kuzingatia, wawe na umri wa zaidi ya miaka 18,” alisema Mkanda.

NA DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply