Wasomaji wa Magazeti Waonjeshwa Utamu wa Spoti Xtra jijini Dar
WASOMAJI wa magazeti ya Global Publishers, leo Februari 14, 2018 wameonjeshwa utamu wa Gazeti jipya la michezo la Spoti Xtra baada ya kugawiwa bure kwa wasomaji hao katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar.
Katikza zoezi hilo la kuwaonjesha utamu wa Spoti Xtra, lilianzia katika maeneo ya Ubungo mawasiliano, kituo cha mabasi Simu 2000, Ubungo River Side, tabata Arona, Baracuda na kumalizia katika mitaa ya Kinyerezi.
Akiwaelezea wasomaji hao, Meneja Masoko wa Global Publishers, Gasper alisema kuwa Gazeti la Spoti Xtra ndilo gazeti bora zaidi kwa sasa Tanzania lenye habari bora, uchambuzi makini na takwimu zote za mchezo wa soka kwa ligi za hapa nchini na Bara la Ulaya.
Wasomaji hao walipata fursa ya kubaini uhondo uliomo ndani ya gazeti hilo zikiwemo makala bomba na stori za kipekee.
Gazeti l Spoti Xtra linakuwa mtaani kwako kila Jumapili kwa bei ya Tsh. 500/= tu.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS | GLOBAL PUBLISHERS
Comments are closed.