The House of Favourite Newspapers

Waumini 11 Wa Kanisa Wafariki Kwa Njaa Wakiwa Kwenye Mfungo – Video

0


Jeshi la Polisi nchini Kenya wamefukua miili ya watu 21 ambao ni waumini wa kanisa la News International Church, ambao inadaiwa wamefariki dunia kwa njaa baada ya kufuata maelekezo ya mchungaji wao ya kufunga mfululizo.

Mchungaji Paul Makenzie Nthenge ndiye anayedaiwa kuwapa maelekezo hayo waumini wake, ikidaiwa kwamba aliwaambia wakifunga mfululizo, wataenda kuonana ana kwa ana na Yesu.

Tayari mchungaji huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini humo huku taarifa zikieleza kwamba huenda makaburi mengine yakabainika.

⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: http://ndstream.net/globalradio/

⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8
⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

Leave A Reply