The House of Favourite Newspapers

Waziri Kitwanga Naye Aikana Kampuni ya Lugumi

0

kitwanga8Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga.

WAKATI Sakata lililoibuliwa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Kampuni ya Lugumi iliyoingia mkataba wa Sh 37 bilioni na Jeshi la Polisi wa kufunga mashine za kielektroniki za kuchukua alama za vidole nchi nzima na kubainika kutotimiza matakwa ya mkataba wake baada ya kufunga mashine 14 tu kati ya 108 ilizotakiwa kufunga, licha ya kulipwa  asilimia 99 ya fedha kwa mujibu wa mkataba, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga amesema hana uhusiano wowote na kampuni hiyo kama watu wanavyodai.
Kitwanga ambaye alihusishwa na Lugumi kupitia kampuni ya Infosys iliyodai kwamba kiongozi huyo ni mmoja wa wanahisa wakati akiwa mfanyakazi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ameeleza kuwa hahusiki na wala halijui suala la Lugumi.

Infosys ambayo imekanusha kuhusika katika sakata hilo imedaiwa kuwa iliisaidia kampuni ya Lugumi kupata vifaa kutoka kampuni ya Dell ya Marekani ili viweze kufungwa kwenye vituo vya polisi.

Jana, Kitwanga alisema anashangazwa kwa jinsi anavyohusishwa kwa maelezo kuwa wakati tukio hilo likitokea mwaka 2011, yeye hakuwa waziri wa wizara hiyo.

WabungeLugumi.

Alichokizungumza Waziri Kitwanga

“Inanishangaza sana sihusiki na wala silijui hili suala la Lugumi. Wakati linatokea sikuwa waziri wa wizara hii ndiyo maana huwa sipendi na wala sitaki kuzungumza chochote kuhusu Lugumi,” alisema.

Kitwanga alifafanua kuwa baadhi ya mambo yameanza kubainika baada ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, licha ya kutotaka kuweka wazi kama suala la Lugumi ni miongoni mwa mambo hayo.

Kamishi-wa-Kanda-Maalu-ya-Dar-Es-Salaam-Suleiman-Kova-akitoa-ufafanuzi-juu-ya-kifo-cha-Sista-kilichotokea-jana-maeneo-ya-Ubungo-kwa-kuuwawa-na-Majambazi-600x360Kamanda Mstaafu wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova

Alichokizungumza Kamanda Kova

Jana Jumanne, Gazeti la Uwazi linalochapishwa na Kampuni ya Global Publishers, lilichapisha habari kuhusu Kamanda Mstaafu wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova kuibuka na kusema kuwa hatambui chochote kuhusu sakata la Lugumi.

“Mimi nilikuwa nashughulika na wahalifu na Lugumi hakuwa mhalifu, siwezi kumzungumzia lolote kwa sababu mimi nimeshastaafu. Huku nilipo sipati taarifa zozote za kiofisi, nimekuwa kama samaki nje ya maji, sina nguvu zozote,” alisema kamanda huyo.

Aliongeza: “Lakini Lugumi namfahamu ila si kwa hilo sakata la vifaa vya kuchukulia alama za vidole ndugu yangu.”

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) ya mwaka 2013/14 ndiyo iliyofichua udhaifu huo. Utekelezwaji wa mkataba huo uliwasilishwa jana kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na mwenyekiti wake Aeshi Hilaly alisema wameanza kuupitia na watakapokamilisha wataweka kila kitu wazi.

ndugai Spika wa Bunge, Job Ndugai

Alichokizungumza Spika wa Bunge, Ndugai

Kwa upande wake Ndugai alipotakiwa kuzungumzia suala hilo alisema,  “Mimi sijapata taarifa zozote za Lugumi. Jambo hilo bado lipo katika kamati ya bunge.”

STORY ZILIZOPITA KUHUSU SAKATA LA LUGUMI

SIKILIZA VIDEO YA MAHOJIANAO NA KAMPUNI YA INFOSYS

Leave A Reply