Waziri Mwakyembe Azindua Mbio Za Marathon
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Mhe Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua rasmi mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon za 18 huku akitoa wito kwa Watanzania kushiriki mbio hizo.
Akizungumza katika Hoteli ya Best Western Coral Beach, Waziri Mwakyembe amewapongeza wadhamini wa mbio hizo wakiongozwa na Kilimanjaro Premium Lager waliodhamini mbio za Km 42.
Tigo Km 21 na Grand Malt waliodhamini mbio za Km 5.
Ameendelea mashindano haya yanazidi kutia moyo sana ambapo sasa hivi yana washiriki zaidi ya 11,000 kutoka zaidi ya nchi 56 kote duniani.
“Hili ni jambo zuri sana kwa taifa kwani tunapata fedha za kigeni kutokana na matumizi yanayofanywa na wageni wakati wa mashindano hayo”. Alisema Waziri Mwakyembe.
Katika mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika mkoani Kilimanjaro, Machi mwakani, mshindi wa jumla atajinyakulia kitita cha shilingi milioni nne na ushindi huo ukienda kwa Mtanzania ataongezewa milioni moja na nusu hivyo kupewa milioni tano na nusu.
PICHA: RICHARD BUKOS /GPL
Comments are closed.