Waziri Ummy Mwalimu Akanusha Kupata Corona
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amekanusha taarifa iliyosambaa mitandaoni kwamba ameambukizwa virusi vya corona.
Kwa mujibu wa taarifa ya wizara yake na akaunti yake ya instagram, Ummy amesema taarifa hiyo haina ukweli na inapaswa kupuuzwa.