The House of Favourite Newspapers

Wema, Idris waoneshana mahaba live Ikulu

0

Mastaa wa Bongo, Idriss Sultan na Wema Sepetu wakikumbatiana.

Richard Bukos

MASTAA wa Bongo, Idriss Sultan na Wema Sepetu, Alhamisi iliyopita walikuwa kwenye Ikulu ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli wakionesha mahaba yao hadharani.

Mastaa hao ambao mara kadhaa wamekuwa wakikanusha vikali kuwa na uhusiano wa kujifunika shuka moja lakini mapozi yao ndiyo yalisababisha wawe gumzo ndani ya ikulu hiyo iliyopo Magogoni jijini Dar ambapo kulikuwa na hafla ya kumpongeza rais huyo baada ya kuapishwa.

Katika tukio hilo wawili hao bila soni walionekana kuzunguuka kwenye viwanja vya ikulu hiyo wakiwa wamekumbatiana kama bibi na bwana hali iliyozidi kukoleza minong’ono kwenye viwanja hivyo.

Paparazi wetu alipotaka kuzungumza na wawili hao kama wangeweza kukiri kwa mara ya kwanza kuwa na uhusiano wa shuka moja, waliombwa waachwe washerekee kwani ndicho kilichowapeleka baada ya kumsaidia kampeni mgombea huyo kwa muda mrefu.

“Pliiiz paparazi naomba hebu tuache jamani kwa kushikana hivi wewe umekutafsiri vipi, mbona ni kawaida tu, huyu mimi ni rafiki yangu namheshimu sana,” alisema Wema.

Leave A Reply