The House of Favourite Newspapers

Wema, Wolper, Aunt Ezekiel Kupofuka

STORI: Na Gladness Mallya na Imelda Mtema | Risasi Jumatano

DAR ES SALAAM: Mtindo wa maisha ya kisasa kwa wasichana Bongo, yamedaiwa kuwa yatasababisha upofu kwa akina dada kadhaa, wakiwemo Wema Sepetu, Jacqueline Walper Masawe ‘Wolper’, Aunt Ezekiel na wenzao kwa sababu ya kuvaa macho bandia pasipo ushauri wa daktari.

Katika siku za hivi karibuni, umezuka mtindo wa wasichana wa kisasa kujipamba kwa urembo wa aina mbalimbali, lakini sasa, wameanza kuvaa macho bandia machoni mwao na hivyo kuyafanya kuonekana kama ni ya kizungu.

Risasi Mchanganyiko lilifanya jitihada za kuwatafuta wataalamu wa afya, hususan macho na kufanikiwa kukutana na daktari Godfrey Chale, ambaye baada ya kuelezwa suala hilo, alitoa ufafanuzi kuhusu kitu kinachoweza kuwakuta watu wote wanaopenda kuvaa macho hayo ya bandia.

“Kuna kitu kinaitwa Conduct Lance, hizi zinatolewa hospitali kwa watu wenye uhitaji nazo. Huwekwa na madaktari kwa namna ambayo inamfanya mvaaji awe comfortable (ajisikie vizuri), kama hawa watakuwa wanapatiwa huduma hiyo hospitalini haina tatizo, lakini kama wanavaa kienyeji, iwe saluni au nyumbani, ni hatari kubwa kwao.

Wema

“Macho ya kila mmoja yana namba na nguvu tofauti ndiyo maana hata wanaovaa miwani wanapaswa kupimwa ili kujua watapewa miwani namba ngapi.

“Kila mtu macho yake yana nguvu tofauti, kwa hiyo unapopimwa, wanajua upewe miwani ipi, sasa ile wanayovaa wao haina tofauti na miwani, kwa hiyo wanapaswa kupimwa ili ziwe sawa na nguvu za macho yao.

“Ukivaa miwani bila kujua nguvu za macho yako ni hatari kwa sababu kama lensi zina nguvu, zinaua macho yako. Unajua kadiri mtu anavyokua, ndivyo nguvu ya viungo mbalimbali mwilini vinavyopungua nguvu zake. Sasa kama nguvu ya macho yako ni ndogo au kubwa na unavaa miwani yenye nguvu kubwa au ndogo, inaua macho yako.

Aunty Ezekiel

“Kwa hiyo uwezekano mkubwa wa macho hayo kwisha nguvu ndani ya muda mfupi. Mbaya zaidi kama macho hayo wanajiwekea wenyewe bila utaalamu, wanahatarisha afya ya macho yao,” alisema daktari huyo.

Mtaalam huyo alisema hata miwani za jua zinazovaliwa, wahitaji wanashauriwa kwenda kununua katika maduka yenye wataalam badala ya kununua barabarani. Alisema katika maduka hayo, zipo ambazo ni salama kutokana na vipimo.

Wolper

“Maana pia kuna miwani zingine zipo ambazo zinabadilika kulingana na hali. Wakati wa jua zinageuka kuwa nyeusi kama ya jua na usiku zinakuwa za kawaida, ndiyo maana unaona kuna watu wanavaa miwani hadi usiku, ni hizi za namna hii,” alisema Dk Chale.

Wakizungumzia kuhusu madhara ya uvaaji wa macho hayo bandia, baadhi ya mastaa walieleza kushtushwa kwao na athari hizo, huku wengine wakisema siyo rahisi wao kudhurika, kwa vile wanatumia za bei mbaya.

Muigizaji wa filamu ambaye pia ni video queen, anayejulikana kama Lulu Mdogo, alisema mara chache huvaa macho hayo katika ishu maalum, ingawa anajua kuwa yana madhara.

Kwa upande wake, Lulu Diva alikiri kuwa mpenzi wa kuvaa macho hayo na kuweka wazi kuwa yamekuwa yakimpa taabu kwani macho yake huuma mara kwa mara. Shoga wa zamani wa Wema Sepetu, Muna ambaye pia huvaa macho hayo, alisema amefanya hivyo mara nyingi na hajawahi kuona jambo lolote baya juu ya macho hayo.

“Macho ninayovaa mimi ni ya kiwango cha juu, hayana madhara kabisa, yapo poa tu,” alisema.

Aunt Ezekiel naye pia alisema ni miongoni mwa wavaaji wakubwa wa macho hayo na kwa muda wote hajawahi kupata madhara ya aina yoyote huku Wolper akisema ameanza muda mrefu kuyavaa hajaona madhara kwa kile alichodai ni kwa vile yake huwa ni ya kiwango cha juu kuliko wengine.

Comments are closed.