The House of Favourite Newspapers

Yacouba Atua Tunisia, Apewa Daktari Bingwa

0

MJUMBE wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Injinia Hersi Said, amesema kuwa kiungo wao mshambuliaji Mburkinabe, Yacouba Songne, anaweza kupona haraka na kurejea uwanjani kutokana na uhodari
wa daktari Mtunisia
atakayemtibu majeraha yake.

 

Yacouba alipata majeraha ya goti katika mchezo uliopita wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting uliochezwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.


Majeraha huyo yalimsababishia
ashindwe kumalizia mchezo huo wa kirafiki katika kipindi cha kwanza cha mchezo
huo na nafasi yake
kuchukuliwa na Mrundi, Said Ntibazonkiza ‘Saido’.


Akizungumza na
Championi Ijumaa, Said alisema kuwa mshambuliaji huyo tayari amefika Tunisia salama
akiwa ameambatana
na daktari wa timu hiyo, Youssef Mohamed na haraka ataanza kupatiwa matibabu.

“Yacouba ameondoka nchini jana (juzi) kuelekea Tunisia ambako amekwenda kwa ajili ya matibabu ya
goti lake aliyoyapata katika mchezo
dhidi ya Ruvu.


“Amekwenda kupatiwa matibabu
nchini humo baada ya kujiridhisha kupitia watalaamu wetu kwamba
kuna daktari bingwa ambaye
atamaliza tatizo lake.


“Ndani ya Yanga hivi sasa
tuna daktari wa viungo bora ambaye amefanya kazi nchini Tunisia, Youssef (Ammar)
katika klabu kubwa za pale na
akishirikiana na kocha wetu, hivyo wametuthibitishia daktari ambaye
atakwenda kumtibu Yacouba
atamaliza tatizo lake,” alisema Said.

Stori: Wilbert Molandi, Dar es Salaam | Championi Ijumaa

Leave A Reply