The House of Favourite Newspapers

Yanga, GSM Watoa Msaada Kwa Anna Majaliwa Tabata

0

KLABU ya Yanga kupitia kwa mdhamini wao Kampuni ya GSM leo Januari 30, 2019 wamefanikisha kutoa masaada wa fedha mahitaji ya chakula cha miezi mitatu pamoja na kugharimia matibabu ya Anna Majaliwa.

 

Yanga imetoa msaada huo kwenye familia ya Anna ambaye anasumbuliwa na tatizo la mwili kukosa fahamu ndani ya miaka mitatu jambo lililompelekea kushindwa kupata choo kwa zaidi ya miezi sita.

 

Akizungumza Anna amesema kuwa alipatabtatizo hilo kwa zaidi ya miaka hiyo mitatu jambo linalomfanya kupata tabu kila kukicha hivyo anawashukuru sana Yanga kupitia mdhamini wao GSM kwa kutambua tatizo lake.

“Najisiki faraja sana kuiona timu yangu Yanga kupitia kwa mdhamini GSM, ambao kwa namna kubwa wametambua tatizo langu na kujitolea msada huu wa chakula pamoja na godoro ambalo kiukweli sikuwa nalo nasikuwa na uwezo wa kununu,”

“Mbali na hivyo pia nimpongeze sana Naibu Meya wa jiji la Dar es Salaam, Abdallah Mtinika kwa kujitolea kufufua bima yangu ambayo iliisha na nikashindwa kuifufua, ila GSM nawashukuru zaidi kwa kuahidi kushughulikia tatizo langu hadi nitakapopona,” alisema Anna.

Kwa upanda wa Afisa Mhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz, amesema kuwa, mbali na misaada iliyotoleo jana poa GSM itahakikisha inampatia matatibabu Anna hata nje ya nchi huku ikimhudumia chakula kwa muda wa miezi mitatu

Leave A Reply