The House of Favourite Newspapers

Yanga vs Simba…Wanaume Wa Kuchungwa

0
Kikosi cha timu ya Yanga.

 

WAKATI timu za Yanga na Simba ziki­tarajiwa kuvaana Jumamosi, Okto­ba 28, mwaka huu, macho ya mashabiki wengi wa soka wa klabu hizi kubwa yapo kwa baadhi ya nyo­ta kadhaa ambao wameonekana mwiba hasa ka­tika michezo hiyo saba ya mzunguk o wa kwanza a m b a y o t a y a r i i m ­echezwa.

Kikosi cha timu ya Simba.

 

Simba na Yanga zi­mecheza michezo saba na zina alama 15 kila mmoja huku zikitofau­tiana katika mabao ya kufunga na kufungwa na zikiendelea kuchuana kwa hali ya juu licha ya ligi kuonekana kuwa bado mbichi.

 

Wafuatao ni kati ya wachezaji ambao wamewe­za kuonyesha uwezo wa hali juu katika michezo iliyo­pita na kwenye pambano baina ya vikosi hivi viwili Ju­mamosi hii wana kazi kubwa ya kuchungwa, lakini pia ndiyo wa­takuwa nyota ambao watafua­tiliwa kwa ukaribu na mashabiki.

Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi.

IBRAHIM AJIBU – YANGA

Amekuwa mwiba kwa sasa kutokana na uwezo anaouonyesha hasa kwa upande wa upachikaji mabao am­bapo tayari katika michezo saba ya Yanga amefunga mabao matano na kui­fanya timu hiyo kuwa sawa kwa pointi 15 na Simba.

Kwa mabeki wa Simba wanatakiwa kuwa macho kwa sababu ana uwezo mkubwa wa ku­badilisha matokeo hasa kwenye mambo aliyoyafanya kwenye mechi mechi na Njombe Mji na Stand United. Msimu uliopita alikuwa Simba.

Washambuliaji wa Yanga wakishangilia kwa pamoja.

EMMANUEL OKWI-SIMBA

Kwa sasa straika huyu Mganda amebatizwa jina la mwa­naume wa Dar kutokana na mabao yake yote nane kufunga jijini Dar.

Kasi na uwezo wa ku­funga unamfanya naye achungwe na wapinzani kwani tangu arejee katika kikosi hicho ambacho aliach­a n a nayo msimu wa 2014/15, mpaka sasa ndiye kinara wa mabao katika Ligi Kuu Bara.

Wachezaji wa timu ya Simba.

OBREY CHRI­WA- YANGA

Mzambia huyo ni mmoja kati ya washambuliaji ambao wame­kuwa tegem­ezi kwa Yan­ga msimu huu ingawa bado kuna w a c h e ­zaji wageni kwenye nafasi a n a y o c h e z a kama Amissi T a m ­b w e r a i a w a B u ­run­d i n a Mz­i m ­b a ­b w e , Don­ald Ngoma ambao msimu huu wamekum­bwa na majeraha tofauti na msimu uliopita, naye kama Ajibu ni moto wa kuotea mbali kwa sababu ya uwezo anaouonyesha.

SHIZA KICHUYA-SIMBA

Tangu atue k a t i k a k i k o s i c h a S im­b a m s i m u uliopita amekuwa ni mmoja kati ya wachezaji ambao wana rekodi ya kuifunga Yanga. Msimu uliopita mchezo wa awali wali­otoka sare ya 1-1 ndiye ali­funga bao hilo na mzunguko wa pili Simba ilishinda mabao 2-1 na alifunga bao moja, ni wazi ni mmoja kati ya wachezaji ambao wame­kuwa wakiinyima usingizi timu ya Yanga msimu huu.

Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma (katikati).

HARUNA NIY­ONZIMA- SIM­BA

Katika mchezo wa Jumamosi kiungo huyu matata ni laz­ima atataka kuonye­sha makali yake kwa wapinzani hao am­bao msimu uliopita alikuwa akiwatumikia kwa kiwango cha hali ya juu. Niyonzima anatazamiwa kuta­zamwa kwa jicho la kitofauti kwa sababu kwanza anakutana na timu yake ya za­mani hivyo watataka kuona nini anakifan­ya ukizingatia hana kiwango kizuri tangu atue Simba.

 

PIUS BUSWITA – YANGA

Kiungo huyu ni wazi ha­sira zake huenda zikai­shia kwa Simba baada ya kukosa mechi kadhaa za awali kutokana na kuwa na utata kwenye usajili wake na mechi ambazo amecheza hivi karibu ameonyesha ki­wango cha hali juu na amei­fungia bao moja pekee.

MAKALA: MARTHA MBOMA | CHAMPIONI JUMATANO

Leave A Reply