The House of Favourite Newspapers

Yanga Yaitungua Lipuli, Tazama Bao la Makambo – Video

Timu ya Yanga imeendeleza moto wake ndani ya Ligi kuu baada ya kufankiwa kushinda mchezo wake wa leo dhidi ya Lipuli uliochezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Yanga wamecheza michezo tisa mpaka sasa wakiwa wameshinda michezo nane na kutoa sare mchezo mmoja tu dhidi ya Simba.

Mchezo huo ambao Lipuli walizidiwa maarifa kipindi cha kwanza baada ya kuweza kuruhusu bao la mapema lililofungwa na Herietier Makambo dakika ya tisa baada ya kupokea pasi kutoka kwa Mrisho Ngassa.

Ushindi huo unawarejesha nafasi ya pili ambayo ilikuwa imekaliwa na Simba, Yanga wamecheza michez 9 na kujikusanyia pointi 25 huku Simba wakiwa na Pointi 23 na vinara wa ligi Azam wamekusanya pointi 27.

GOLI la MAKAMBO YANGA VS LIPULI 1 -0

Comments are closed.